@furqanbot

@furqanbot


فَمَا لَنَا مِن شَافِعِينَ ﴿١٠٠﴾

100. “Basi hatuna waombezi wowote.

 

 

 

وَلَا صَدِيقٍ حَمِيمٍ ﴿١٠١﴾

101. “Na wala rafiki khalisi.

 

 

 

فَلَوْ أَنَّ لَنَا كَرَّةً فَنَكُونَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ﴿١٠٢﴾

102. “Basi lau tungelikuwa tuna fursa ya kurudi (duniani) tungekuwa miongoni mwa Waumini.”

 

 

 

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٠٣﴾

103. Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٠٤﴾

104. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

كَذَّبَتْ قَوْمُ نُوحٍ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٠٥﴾

105. Watu wa Nuwh walimkadhibisha Rusuli.

 

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ﴿١٠٦﴾

106. Alipowaambia ndugu yao Nuwh: “Je, hamtokuwa na taqwa?”

 

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٠٧﴾

107. “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٠٨﴾

108. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٠٩﴾

109. “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١١٠﴾

110. “Basi mcheni Allaah na nitiini.”

 

 

 

قَالُوا أَنُؤْمِنُ لَكَ وَاتَّبَعَكَ الْأَرْذَلُونَ﴿١١١﴾

111. Wakasema: “Je, tukuamini na hali kuwa waliokufuata ni wadhalilifu?”

 

 

 

قَالَ وَمَا عِلْمِي بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١١٢﴾

112.  Akasema: “Na najuaje kwa ambayo waliyokuwa wanayatenda?

 

 

 

إِنْ حِسَابُهُمْ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّي ۖ لَوْ تَشْعُرُونَ ﴿١١٣﴾

113. “Hesabu yao haiko isipokuwa kwa Rabb wangu, lau mngetambua.

 

 

 

وَمَا أَنَا بِطَارِدِ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١٤﴾

114. “Nami sitowafukuza walioamini.

 

 

 

إِنْ أَنَا إِلَّا نَذِيرٌ مُّبِينٌ ﴿١١٥﴾

115. “Mimi si yeyote ila mwonyaji dhahiri.”

 

 

 

قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا نُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمَرْجُومِينَ ﴿١١٦﴾

116. Wakasema: “Usipoacha ewe Nuwh bila shaka utakuwa miongoni mwa wenye kurajimiwa.”

 

 

 

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوْمِي كَذَّبُونِ ﴿١١٧﴾

117. Akasema: “Rabb wangu! Hakika watu wangu wamenikadhibisha.

 

 

 

فَافْتَحْ بَيْنِي وَبَيْنَهُمْ فَتْحًا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿١١٨﴾

118. “Basi Hukumu baina yangu na baina yao hukumu (Yako), na Uniokoe mimi na wale walio pamoja nami miongoni mwa Waumini.”

 

 

 

فَأَنجَيْنَاهُ وَمَن مَّعَهُ فِي الْفُلْكِ الْمَشْحُونِ ﴿١١٩﴾

119. Tukamuokoa pamoja na wale waliokuwa naye katika jahazi iliyosheheni.

 

 

 

ثُمَّ أَغْرَقْنَا بَعْدُ الْبَاقِينَ ﴿١٢٠﴾

120. Kisha Tukawagharikisha baada ya hapo waliobakia.

 

 

 

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٢١﴾

121.  Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٢٢﴾

122. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye Nguvu, Mshindi Asiyeshindika, Mwenye Kurehemu.

 

 

 

كَذَّبَتْ عَادٌ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٢٣﴾

123. Kina ‘Aad walimkadhibisha Rusuli.

 

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ﴿١٢٤﴾

124. Alipowaambia ndugu yao Huwd: “Je, hamtokuwa na taqwa?”

 

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٢٥﴾

125. “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٢٦﴾

126. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٢٧﴾

127. “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

 

أَتَبْنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ آيَةً تَعْبَثُونَ ﴿١٢٨﴾

128. “Je, mnajenga katika kila sehemu maarufu za mnyanyuko, majengo marefurefu kwa ajili ya burudani tu?

 

 

 

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمْ تَخْلُدُونَ﴿١٢٩﴾

129. “Na mnafanya mangome madhubuti kama kwamba mtaishi milele?

 

 

 

وَإِذَا بَطَشْتُم بَطَشْتُمْ جَبَّارِينَ ﴿١٣٠﴾

130. “Na mnapokamata kushambulia mnatumia nguvu kwa uadui na ujabari.  

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٣١﴾

131. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَاتَّقُوا الَّذِي أَمَدَّكُم بِمَا تَعْلَمُونَ﴿١٣٢﴾

132. “Na mcheni Ambaye Amekupeni yale mnayoyajua.

 

 

 

أَمَدَّكُم بِأَنْعَامٍ وَبَنِينَ ﴿١٣٣﴾

133. “Amekupeni wanyama wa mifugo na watoto.

 

 

 

وَجَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿١٣٤﴾

134. “Na mabustani na chemchemu.

 

 

 

إِنِّي أَخَافُ عَلَيْكُمْ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ﴿١٣٥﴾

135. “Hakika mimi nakukhofieni adhabu ya Siku adhimu.”

 

 

 

قَالُوا سَوَاءٌ عَلَيْنَا أَوَعَظْتَ أَمْ لَمْ تَكُن مِّنَ الْوَاعِظِينَ ﴿١٣٦﴾

136. Wakasema: “Ni sawa sawa kwetu, ukiwaidhi au usipokuwa miongoni mwa wanaowaidhi.

 

 

 

إِنْ هَـٰذَا إِلَّا خُلُقُ الْأَوَّلِينَ ﴿١٣٧﴾

137. “Haya si chochote isipokuwa ni desturi ya watu wa awali.

 

 

 

وَمَا نَحْنُ بِمُعَذَّبِينَ ﴿١٣٨﴾

138. “Na wala hatutoadhibiwa.”

 

 

 

فَكَذَّبُوهُ فَأَهْلَكْنَاهُمْ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةًۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٣٩﴾

139. Wakamkadhibisha; basi Tuliwaangamiza. Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٤٠﴾

140. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

كَذَّبَتْ ثَمُودُ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٤١﴾

141. Kina Thamuwd walimkadhibisha Rusuli.

 

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ صَالِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ﴿١٤٢﴾

142. Alipowaambia ndugu yao Swaalih: “Je, hamtokuwa na taqwa?”

 

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٤٣﴾

143. “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٤٤﴾

144. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٤٥﴾

145. “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

 

أَتُتْرَكُونَ فِي مَا هَاهُنَا آمِنِينَ ﴿١٤٦﴾

146. “Je, mtaachwa mkiwa katika amani kwenye haya hapa mliyonayo? 

 

 

 

فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ﴿١٤٧﴾

147. “Katika mabustani na chemchemu.

 

 

 

وَزُرُوعٍ وَنَخْلٍ طَلْعُهَا هَضِيمٌ ﴿١٤٨﴾

148. “Na mimea na mitende makole yake laini, yamewiva.

 

 

 

وَتَنْحِتُونَ مِنَ الْجِبَالِ بُيُوتًا فَارِهِينَ﴿١٤٩﴾

149. “Na mnachonga majabalini nyumba kwa uhodari kabisa.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٥٠﴾

150. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَلَا تُطِيعُوا أَمْرَ الْمُسْرِفِينَ ﴿١٥١﴾

151. “Na wala msitii amri ya wenye kupindukia mipaka.

 

 

 

الَّذِينَ يُفْسِدُونَ فِي الْأَرْضِ وَلَا يُصْلِحُونَ ﴿١٥٢﴾

152. “Ambao wanafanya ufisadi katika ardhi na wala hawatengenezi.”

 

 

 

قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ﴿١٥٣﴾

153. Wakasema: “Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.

 

 

 

مَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا فَأْتِ بِآيَةٍ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿١٥٤﴾

154. “Wewe si chochote isipokuwa mtu kama sisi; basi lete Aayah (dalili, muujiza) ukiwa wewe ni miongoni mwa wakweli.”

 

 

 

قَالَ هَـٰذِهِ نَاقَةٌ لَّهَا شِرْبٌ وَلَكُمْ شِرْبُ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ ﴿١٥٥﴾

155. Akasema: “Huyu hapa ngamia jike ana zamu ya kinywaji, nanyi mna zamu ya kinywaji siku maalumu.

 

 

 

وَلَا تَمَسُّوهَا بِسُوءٍ فَيَأْخُذَكُمْ عَذَابُ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٥٦﴾

156. “Na wala msimguse kwa uovu, ikaja kukuchukueni adhabu ya Siku adhimu.”

 

 

 

فَعَقَرُوهَا فَأَصْبَحُوا نَادِمِينَ ﴿١٥٧﴾

157. Basi wakamuua wakapambazukiwa wenye kujuta.

 

 

 

فَأَخَذَهُمُ الْعَذَابُ ۗ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖوَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٥٨﴾

158. Ikawachukuwa adhabu. Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٥٩﴾

159. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ الْمُرْسَلِينَ ﴿١٦٠﴾

160. Watu wa Luwtw walimkadhibisha Rusuli.

 

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ أَخُوهُمْ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ﴿١٦١﴾

161. Alipowaambia ndugu yao Luwtw: “Je, hamtokuwa na taqwa?”

 

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٦٢﴾

162. “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٦٣﴾

163. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٤﴾

164. “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

 

أَتَأْتُونَ الذُّكْرَانَ مِنَ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٥﴾

165. “Je, mnawaendea wanaume miongoni mwa walimwengu?

 

 

 

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمْ رَبُّكُم مِّنْ أَزْوَاجِكُم ۚ بَلْ أَنتُمْ قَوْمٌ عَادُونَ﴿١٦٦﴾

166. “Na mnawaacha wale Aliyekuumbieni Rabb wenu kati ya wake zenu. Bali nyinyi ni watu mliopindukia mipaka.”

 

 

 

قَالُوا لَئِن لَّمْ تَنتَهِ يَا لُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ الْمُخْرَجِينَ ﴿١٦٧﴾

167. Wakasema: “Usipoacha ee Luwtw, bila shaka utakuwa miongoni mwa watakaofukuzwa.”

 

 

 

قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ الْقَالِينَ ﴿١٦٨﴾

168. Akasema: “Hakika mimi ni katika wanaochukia mno kitendo chenu.

 

 

 

رَبِّ نَجِّنِي وَأَهْلِي مِمَّا يَعْمَلُونَ ﴿١٦٩﴾

169. “Rabb wangu! Niokoe na ahli zangu kutokana na yale wanayotenda.”

 

 

 

فَنَجَّيْنَاهُ وَأَهْلَهُ أَجْمَعِينَ ﴿١٧٠﴾

170. Basi Tukamuokoa na ahli zake wote.

 

 

 

إِلَّا عَجُوزًا فِي الْغَابِرِينَ ﴿١٧١﴾

171. Isipokuwa kikongwe katika waliobaki nyuma.

 

 

 

ثُمَّ دَمَّرْنَا الْآخَرِينَ ﴿١٧٢﴾

172. Kisha Tukadamiri wengineo.

 

 

 

وَأَمْطَرْنَا عَلَيْهِم مَّطَرًا ۖ فَسَاءَ مَطَرُ الْمُنذَرِينَ ﴿١٧٣﴾

173. Na Tukawanyeshea mvua (ya adhabu). Basi uovu ulioje mvua ya walioonywa.

 

 

 

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٧٤﴾

174. Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٧٥﴾

175. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

كَذَّبَ أَصْحَابُ الْأَيْكَةِ الْمُرْسَلِينَ﴿١٧٦﴾

176. Watu wa Al-Aykah wamemkadhibisha Rusuli.

 

 

 

إِذْ قَالَ لَهُمْ شُعَيْبٌ أَلَا تَتَّقُونَ ﴿١٧٧﴾

177. Alipowaambia Shu’ayb: “Je, hamtokuwa na taqwa?”

 

 

 

إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ﴿١٧٨﴾

178. “Hakika mimi kwenu ni Rasuli mwaminifu.

 

 

 

فَاتَّقُوا اللَّـهَ وَأَطِيعُونِ ﴿١٧٩﴾

179. “Basi mcheni Allaah na nitiini.

 

 

 

وَمَا أَسْأَلُكُمْ عَلَيْهِ مِنْ أَجْرٍ ۖ إِنْ أَجْرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٨٠﴾

180. “Na wala sikuombeni ujira wowote juu yake. Ujira wangu hauko isipokuwa kwa Rabb wa walimwengu.”

 

 

 

أَوْفُوا الْكَيْلَ وَلَا تَكُونُوا مِنَ الْمُخْسِرِينَ ﴿١٨١﴾

181. “Timizeni kipimo na wala msiwe miongoni mwa wenye kupunja.

 

 

 

وَزِنُوا بِالْقِسْطَاسِ الْمُسْتَقِيمِ ﴿١٨٢﴾

182. “Na pimeni mizani kwa uadilifu iliyosawa.

 

 

 

وَلَا تَبْخَسُوا النَّاسَ أَشْيَاءَهُمْ وَلَا تَعْثَوْا فِي الْأَرْضِ مُفْسِدِينَ ﴿١٨٣﴾

183. “Na wala msiwapunje watu vitu vyao, na wala msieneze uovu katika ardhi hali ya kuwa ni wenye kufanya ufisadi.

 

 

 

وَاتَّقُوا الَّذِي خَلَقَكُمْ وَالْجِبِلَّةَ الْأَوَّلِينَ﴿١٨٤﴾

184. “Na mcheni Ambaye Amekuumbeni na viumbe vingi wa awali.”

 

 

 

قَالُوا إِنَّمَا أَنتَ مِنَ الْمُسَحَّرِينَ ﴿١٨٥﴾

185. Wakasema: “Hakika wewe ni miongoni mwa waliorogwa.

 

 

 

وَمَا أَنتَ إِلَّا بَشَرٌ مِّثْلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ الْكَاذِبِينَ ﴿١٨٦﴾

186. “Nawe si chochote isipokuwa ni mtu kama sisi, na hakika tunakudhania ni miongoni mwa waongo.

 

 

 

فَأَسْقِطْ عَلَيْنَا كِسَفًا مِّنَ السَّمَاءِ إِن كُنتَ مِنَ الصَّادِقِينَ ﴿١٨٧﴾

187. “Basi tuangushie vipande vipande vya mbingu, ukiwa ni miongoni mwa wakweli.”

 

 

 

قَالَ رَبِّي أَعْلَمُ بِمَا تَعْمَلُونَ ﴿١٨٨﴾

188. Akasema: “Hakika Rabb wangu Anajua zaidi yale mnayoyatenda.”

 

 

 

فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمْ عَذَابُ يَوْمِ الظُّلَّةِ ۚإِنَّهُ كَانَ عَذَابَ يَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿١٨٩﴾

189. Wakamkadhibisha; basi adhabu ya siku ya kivuli (cha mawingu) ikawachukua. Hakika hiyo ilikuwa ni adhabu ya Siku kubwa mno.

 

 

 

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَآيَةً ۖ وَمَا كَانَ أَكْثَرُهُم مُّؤْمِنِينَ ﴿١٩٠﴾

190. Hakika katika hayo pana Aayah (ishara, zingatio n.k.), lakini wengi wao hawakuwa wenye kuamini.

 

 

 

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ﴿١٩١﴾

191. Na hakika Rabb wako bila shaka Ndiye Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

وَإِنَّهُ لَتَنزِيلُ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٩٢﴾

192. Na hakika hii (Qur-aan) ni uteremsho wa Rabb wa walimwengu.

 

 

 

نَزَلَ بِهِ الرُّوحُ الْأَمِينُ ﴿١٩٣﴾

193. Ameiteremsha haya Ar-Ruwh (Jibriyl) mwaminifu.

 

 

 

عَلَىٰ قَلْبِكَ لِتَكُونَ مِنَ الْمُنذِرِينَ﴿١٩٤﴾

194. Juu ya moyo wako (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) ili uwe miongoni mwa waonyaji.

 

 

 

بِلِسَانٍ عَرَبِيٍّ مُّبِينٍ ﴿١٩٥﴾

195. Kwa lugha ya Kiarabu bayana.

 

 

 

وَإِنَّهُ لَفِي زُبُرِ الْأَوَّلِينَ ﴿١٩٦﴾

196. Na hakika hii bila shaka imo katika Vitabu vya awali.

 

 

 

أَوَلَمْ يَكُن لَّهُمْ آيَةً أَن يَعْلَمَهُ عُلَمَاءُ بَنِي إِسْرَائِيلَ ﴿١٩٧﴾

197. Je, haikuwa kwao ni Aayah (ishara, dalili), kwamba waitambue wanavyuoni wa wana wa Israaiyl? 

 

 

 

وَلَوْ نَزَّلْنَاهُ عَلَىٰ بَعْضِ الْأَعْجَمِينَ﴿١٩٨﴾

198. Na lau Tungeliiteremsha (hii Qur-aan) juu ya yeyote miongoni mwa wasio Waarabu.

 

 

 

فَقَرَأَهُ عَلَيْهِم مَّا كَانُوا بِهِ مُؤْمِنِينَ﴿١٩٩﴾

199. Na akawasomea, wasingelikuwa wenye kuiamini.

 

 

 

كَذَٰلِكَ سَلَكْنَاهُ فِي قُلُوبِ الْمُجْرِمِينَ﴿٢٠٠﴾

200. Hivyo ndivyo Tunavyoingiza katika nyoyo za wakhalifu.

 

 

 

لَا يُؤْمِنُونَ بِهِ حَتَّىٰ يَرَوُا الْعَذَابَ الْأَلِيمَ ﴿٢٠١﴾

201. Hawaiamini mpaka waione adhabu iumizayo.

 

 

 

فَيَأْتِيَهُم بَغْتَةً وَهُمْ لَا يَشْعُرُونَ﴿٢٠٢﴾

202. Basi itawajia kwa ghafla, nao hawatambui.

 

 

 

فَيَقُولُوا هَلْ نَحْنُ مُنظَرُونَ ﴿٢٠٣﴾

203. Kisha watasema: “Je, sisi tutapewa muhula?”

 

 

 

أَفَبِعَذَابِنَا يَسْتَعْجِلُونَ ﴿٢٠٤﴾

204. Je, wanahimiza adhabu Yetu?

 

 

 

أَفَرَأَيْتَ إِن مَّتَّعْنَاهُمْ سِنِينَ ﴿٢٠٥﴾

205. Je, unaonaje kama Tukiwastarehesha miaka.

 

 

 

ثُمَّ جَاءَهُم مَّا كَانُوا يُوعَدُونَ ﴿٢٠٦﴾

206. Kisha ikawajia yale waliyokuwa wameahidiwa.

 

 

 

مَا أَغْنَىٰ عَنْهُم مَّا كَانُوا يُمَتَّعُونَ﴿٢٠٧﴾

207. Hayatowafaa yale waliyokuwa wakistarehe nayo.

 

 

 

وَمَا أَهْلَكْنَا مِن قَرْيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ﴿٢٠٨﴾

208. Na Hatukuangamiza mji wowote isipokuwa ulikuwa na waonyaji.

 

 

 

ذِكْرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَالِمِينَ ﴿٢٠٩﴾

209.  Ni ukumbusho na Hatukuwa madhalimu.

 

 

 

وَمَا تَنَزَّلَتْ بِهِ الشَّيَاطِينُ ﴿٢١٠﴾

210. Na wala hawakuteremka nayo (hii Qur-aan) mashaytwaan.

 

 

 

وَمَا يَنبَغِي لَهُمْ وَمَا يَسْتَطِيعُونَ﴿٢١١﴾

211. Na wala haipasi kwao na wala hawawezi.

 

 

 

إِنَّهُمْ عَنِ السَّمْعِ لَمَعْزُولُونَ ﴿٢١٢﴾

212. Hakika wao bila shaka wametengwa mbali kuisikiliza.

 

 

 

فَلَا تَدْعُ مَعَ اللَّـهِ إِلَـٰهًا آخَرَ فَتَكُونَ مِنَ الْمُعَذَّبِينَ ﴿٢١٣﴾

213. Basi usiombe pamoja na Allaah mwabudiwa mwengine ukaja kuwa miongoni mwa watakaoadhibiwa.

 

 

 

وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ ﴿٢١٤﴾

214. Na onya (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) jamaa zako wa karibu.

 

 

 

وَاخْفِضْ جَنَاحَكَ لِمَنِ اتَّبَعَكَ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ ﴿٢١٥﴾

215. Na inamisha ubawa wako kwa anayekufuata miongoni mwa Waumini.

 

 

 

فَإِنْ عَصَوْكَ فَقُلْ إِنِّي بَرِيءٌ مِّمَّا تَعْمَلُونَ ﴿٢١٦﴾

216. Wakikuasi; basi sema: “Hakika mimi niko mbali na hayo mnayoyatenda.”

 

 

 

وَتَوَكَّلْ عَلَى الْعَزِيزِ الرَّحِيمِ ﴿٢١٧﴾

217. Na tawakali kwa Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika, Mwenye kurehemu.

 

 

 

الَّذِي يَرَاكَ حِينَ تَقُومُ ﴿٢١٨﴾

218.  Ambaye Anakuona wakati unaposimama.

 

 

 

وَتَقَلُّبَكَ فِي السَّاجِدِينَ ﴿٢١٩﴾

219. Na mageuko yako katika wenye kusujudu. 

 

 

 

إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ﴿٢٢٠﴾

220. Hakika Yeye Ndiye Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote.

 

 

 

هَلْ أُنَبِّئُكُمْ عَلَىٰ مَن تَنَزَّلُ الشَّيَاطِينُ﴿٢٢١﴾

221. Je, nikujulisheni wanaowateremkia mashaytwaan?

 

 

 

تَنَزَّلُ عَلَىٰ كُلِّ أَفَّاكٍ أَثِيمٍ ﴿٢٢٢﴾

222. Wanateremka juu ya kila mzushi mkubwa mwingi wa kutenda dhambi. 

 

 

 

يُلْقُونَ السَّمْعَ وَأَكْثَرُهُمْ كَاذِبُونَ﴿٢٢٣﴾

223. Wanaotega sikio na wengi wao ni waongo.

 

 

 

وَالشُّعَرَاءُ يَتَّبِعُهُمُ الْغَاوُونَ ﴿٢٢٤﴾

224. Na washairi wanafuatwa na wapotofu.

 

 

 

أَلَمْ تَرَ أَنَّهُمْ فِي كُلِّ وَادٍ يَهِيمُونَ﴿٢٢٥﴾

225. Je, huoni kwamba wao katika kila bonde wanatangatanga?

 

 

 

وَأَنَّهُمْ يَقُولُونَ مَا لَا يَفْعَلُونَ ﴿٢٢٦﴾

226. Nao wanasema yale wasiyoyafanya.

 

 

 

إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ وَذَكَرُوا اللَّـهَ كَثِيرًا وَانتَصَرُوا مِن بَعْدِ مَا ظُلِمُوا ۗ وَسَيَعْلَمُ الَّذِينَ ظَلَمُوا أَيَّ مُنقَلَبٍ يَنقَلِبُونَ ﴿٢٢٧﴾

227. Isipokuwa wale walioamini na wakatenda mema, na wakamdhukuru Allaah kwa wingi, na wakapata nusura baada ya kudhulumiwa. Na hivi karibuni watakuja kujua wale waliodhulumu mgeuko gani watakaogeuka.

 

 


Report Page