Simu za Google Pixel sahihi za kununua (2026) | SimuNzuri
TeknolojiaHapa Tanzania Google Pixel imeshika kwa sasa
Ni simu zilizovuta wengi na kununua kama vipofu
Matokeo yake wengine wameibuka kununua Google Pixel ambazo hazifai kwa sasa
Baadhi za Google zina mapungufu upande wa utendaji, software na utunzaji wa chaji
Kwa sababu Pixel nyingi zinazonunuliwa hapa Tanzania ni za zamani
Zijue zipi sahihi usije ukajichanganya huko mbeleni
Hizi hapa Google Pixel Sahihi
Kuna mamilioni ya sababu kwa nini ununue hizi Google Pixel
Na ni nafuu mara mia kuepuka matole kuanzia Google Pixel 4 kwenda chini ikiwezekana
Hizi ndio sababu na naamini utanishukuru kukuepushia hasara mbeleni
Ukubwa wa betri
Simu za Google Pixel ya mwaka 2019 kuja chini zina betri ndogo sana
Kwa mfano Google Pixel 4 ukubwa wa betri ni mAh 2800
Hii betri kiuhalisia haiwezi kudumu na chaji hata kwa masaa nane
Simu nyingi kwa sasa kufikisha masaa 12 ni jambo la kawaida
Kumbuka Google Pixel 4 inakaribia miaka 7 tangu itoke
Hivyo ubora hauwezi kuwa sawa kama awali
Hivyo kama bajeti yako ni chini ya laki tano walau unapaswa ununue Google Pixel 5
Nguvu ya utendaji
Google Pixel zilizotoka mwaka 2021 zina pafomansi kubwa sana
Pamoja na utendaji mkubwa hazitumii kiwango kikubwa cha chaji
Mwaka 2021 Google walianza kutumia prosesa wanazoziunda wao wenyewe
Prosesa hizo Zinaitwa Google Tensor
Zinaambatana na core aina ya Cortex X1 kwa ajili ya kazi zinazohitaji nguvu kubwa
Kwa kufipi kama unataka kuitumia simu kwa mambo mengi basi Google Pixel 6 kwenda mbele chaguo zuri zaidi
Na uzuri bajeti ya hizi simu zipo kati ya 500,000 hadi 600,000
Ukubwa wa RAM
Unajua katika kipindi cha miaka 2 iliyopita simu zinakuja na mifumo mingi ya AI
Mifumo ya AI inatumia sana RAM
RAM ikiwa ndogo baada ya muda simu inaanza kuwa nzito
Google Pixel 3, kwa mfano, ina kiasi cha RAM ya GB 4
Kwa sasa hiki ni kiwango kidogo
Wakati kuanzia Google Pixel 5 zinakuwekea RAM ya GB 8 na kuendelea
Zipo Google Pixel hadi za GB 12
Maboresho ya Software
Simu nzuri ni ile inayotunza thamani yake muda mrefu
Simu inayokupa nafasi ya kuweza kutumia teknolojia mpya kwa kupata toleo jipya la mfumo endeshi
Kuna baadhi ya simu za Google Pixel hazitopoeki tena toleo la android jipya
Kwa sasa Android mpya kabisa ni Android 16
Google Pixel 5 kwa mfano inapokea mwisho Android 14
Wakati huo Google Pixel 6 inapokea Android 16 na matoleo yatakayofuata
Matoleo mapya ya Android huasidia kuboresha pia usalama wa simu
Mifumo ya kamera
Simu za Google Pixel kabla 2020 zina machaguo machache ya aina ya kamera
Kwa mfano Google Pixel 4 ina kamera mbili tu haina kamera aina telephoto
Lakini Google Pixel 6 Pro inakuja na kamera tatu
Huku ikiwa na kamera ya ziada ya lenzi ya ultrawide
Kwa hiyo kwa mpenzi wa kamera hana budi kununua Google Pixel 6 Pro kwenda mbele
Ubora wa display(kioo)
Vioo vya simu miaka hii vya daraja kati vinatumia refresh rate ya 120Hz
Hii inafanya tachi kuwa nyepesi na muonekano mzuri unapo-scroll
Pia Google Pixel za zamani vioo havina muangaza mkubwa
Mara nyingi muangaza huwa ni chini ya nits 1000
Lakini vioo vya goole pixel 6 nits ni kubwa
Na kioo cha hdr10+ hivyo vitu vinaokana kwa kina kikubwa cha rangi