Realme P4 Power – Simu yenye betri kubwa haijawahi tokea | SimuNzuri
TeknolojiaUnatamani kutumia simujanja masaa karibu 24 kwenye intaneti bila kuwaza chaji kuisha?
Kama ni hivyo Realme P4 Power ndio simu sahihi
Realme P4 Power ndio simu ya kwanza kuja na bonge labetri la ukubwa wa mAh 10,001
Ukubwa wake wa betri unaifanya simu kudumu na chaji masaa mengi kwenye kucheza gemu na kutumuia intaneti muda wote
Hata hivyo bei yake pia imechangamka
Bei ya Realme P4 Power GB 128
Kwa hapa Tanzania realme p4 power haijaingia rasmi
Lakini gharama zake mpaka kukufikia inafika laki nane na nusu (850,000)
Inapatikana kwenye masoko ya India
Na ukubwa wa RAM unaanzia GB 8 na zingine GB 12
Kwa hiyo bei inabadilika kutokana na ukubwa wa memori na RAM
Aina ya betri
Ukubwa wa betri wa Realme P4 Power ni mAh 10,001
Mara nyingi simu tunazotumia betri zake huwa na mAh 5000
Ukubwa wa betri umechangiwa na aina mpya betri
Aina hiyo ya betri inatambulika kama silicon cabon
Si/C nishati yake ni kubwa ukilinganisha na betri zilizozoeleka
Hivyo simu nyingi kwa sasa zinaambatana na aina hii ya betri
Usije kushangaa kutokea kwa simu yenye betri kubwa zaidi ya hii
Uwezo wa kukaa na chaji
Simu inaweza kukaa na chaji masaa 14 ukiwa unacheza magemu muda wote
Ukiwa unatumia intaneti muda wote inakaa siku nzima
Kwa sababu ya betri kubwa sana chaji yake inachukuwa muda kujaa
Kutoka 0% hadi 100% inachukua takribani dakika 90
Na chaji yake inaweza kupeleka umeme hadi wa wati 80
Kama ingekuwa ni betri ndogo ya mAh ingechukua karibu dakika 45