Kuoshwa maiti upesi

Kuoshwa maiti upesi

🔙 Home

Katika mambo ya kheri ambayo humfikia maiti ni kufanya upesi katika kumtayarisha kwa kumkosha, kumkafini na kumzika.

 

Katika kuoshwa vinachungwa vifuatavyo:

 

· Idadi ya kuoshwa iwe ni mara tatu na zaidi ikibidi kwa haja kwa sharti kuwa idadi hiyo iwe ni witri: tatu, tano au saba na mfano wa haya.

 

· Itumike majani ya mkunazi au sabuni katika kila anapokoshwa ili kumsafisha vizuri zaidi.

 

· Muoshaji atumie sabuni au mfano wake kama vile siku hizi gloves inavyotumika na kuwepo na sitra yenye kumfunika maiti baada ya kuvuliwa nguo.

 

· Ni vizuri kutia kafuri katika maji haswa katika josho la mwisho au mafuta mazuri maadamu sio haramu, na inapokuwa ni haramu basi hayafai.

 

· Kucha za mwanamke zitapunguzwa na kuoshwa vizuri, hali kadhalika nywele zake kuchanwa na kufungwa vifundo vitatu nyuma yake.

 

·  Aanze kukosha sehemu za kulia kwanza na sehemu za udhu

 

·  Mwanamume hukosha wanaume, mwanamke hukosha wanawake, mume humuosha mkewe na mke humkosha mumewe.

 

·  Shahidi, aliyekufa katika vita hakoshwi.


Report Page