Coca-cola Kuja Na Simu Janja Yao!

Coca-cola Kuja Na Simu Janja Yao!

https://teknolojia.co.tz/coca-cola-kuja-na-simu-janja-yao/?utm_source=rss&utm_medium=rss&utm_campaign=coca-cola-kuja-na-simu-ja


Tumeshaona simu tofauti tofauti ambazo zinakujaga kubeba chapa fulani kwa muda na huo kunakua na matoleo maalamu, mfano


TECNO – (Tecno Camon CX) Toleo La Manchester City



SAMSUNG – (Galaxy Z Flip 4) Toleo la Maison Margiela


OPPO – (Oppo Reno 10X Zoom) Toleo la Barcelona


N.k


Na matoleo mengine mengi tuu ambayo makampuni mengi huwa yanatoa, kwa haraka haraka ni kwamba matoleo haya huwa tayari yapo katika soko na kampuni nyingine huwa inakuja kuweka chapa (brand) yake tuu.


SOMA PIA  WhatsApp kuja na muonekano wa giza

Huwa ni vigumu kabisa kwa kampuni ambayo haijihusishi kabisa katika soko la simu kuja kusikia kuwa imezindua simu yake.


Pengine hili linakuja kubadilishwa na Coca-cola, maana wako mbioni katika kuzalisha simu yao ya kwanza kabisa.


Lakini hata hivyo hili sio la kushangaza sana maana hata miaka kadhaa iliyopita Pepsi nao waliachiwa simu janja mbili Yaani Pepsi P1 na Pepsi P1s japo simu hizi zilikua kwa ajili ya soko la china. Soma zaidi >>HAPA<<


SOMA PIA  YouTube ya kwenye Android na iOS yaboreshwa

Kwa sasa swala hili limetoka kama fununu lakini viashiria vyote vinaonyesha kwamba sio siri tena jambo hili linaenda kufanyika.


Ushahidi kama akaunti ya Twitter ya simu janja hiyo kutoka Coca-cola imefunguliwa na inaitwa @colaphoneglobal lakini vile vile usishangae simu hii nayo ikawa ni kama zile zinazobeba chapa (brand) tuu.


Yaani pengine coca-cola hawatakaa chini na kuanza kutengeneza simu hii kutoka mwanzo  hadi mwisho.


Kwa sasa kuna picha inayosambaa katika mtandao huku ikiwa inayonyesha upande wa nyuma –muonekano wa kamera – bila kuonyesha upande wa mbele wa simu hiyo.


SOMA PIA  Sony Xperia 1: Simu yenye upekee wa aina yake

Kwa sasa hakuna taarifa zozote za undani juu ya simu janja hii na hata bei haipo wazi lakini vyanzo mbalimbali vinadai kuwa itakua ni moja kati ya zile simu janja ambazo haina gharama kubwa


Ningependa kusikia kutoka kwako, niandikie hapo chini katika eneo la comment, je uko tayari kuanza kutumia simu yenye chapa la soda ya Coca-cola?


Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.


Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii


Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn


Hash



Report Page