CHAKULA CHA MTOTO

CHAKULA CHA MTOTO

Dr.Mansura M. Mtibora

Kwanza inabidi tuelewe kuwa mtoto akifikisha miezi sita anatakiwa kuanzishiwa chakula kwani tumbo lake linakua tayari kupokea aina nyingine ya chakula ukiacha mbali na maziwa ya mama pili mtoto anakua hawezi kushiba tena maziwa tu ya mama hata ungemnyonyesha siku nzima bila kupumzika.

unaweza saga kwa mashine au kwa njia yoyote .

Hivyo ni muhimu kupata ndondoo muhimu kuhusu hatua hii ya ukuaji wa mtoto kwani wengi huishia kupata utapiamlo kwa sababu mbalimbali katika uandaji,aina au hata idadi ya mlo wa chakula cha mtoto.

yafuatayo ukiyazingati yatasadia kuimarisha afya ya mwanao

1.Chakula cha mtoto kinatakiwa kuandaliwa kuhifadhiwa na mpaka anapokula katika mazingira yenye usafi wa hali ya juu

2.Usimuachishe mtoto maziwa yako mara tu atakapoanza kula endelea kumnyonyesha

Vyombo na mazingira viwe safi

3.Chakula cha mtoto ni lazima kiwe kamili kwa kuwa na aina za vyakula kama protein ,wanga ,mafuta nani vitamini

4.Kama mwanao anakunywa uji basi usimchamganyie nafaka zaidi ya moja kwenye unga wake bali unaweza kuweka makundi yote ya vyakula kama protein (maziwa) mafuta(blueband), vitamini (karoti)

Nafaka tatu sio nzuri kwani kila nafaka ina muda wake wa kuiva

5.Uji uchemke vizuri kuepuka kutoiva hasa kama unga wake una mchanganyiko wa ulezi,ngano nk

6.Muanzishie mtoto chakula kimoja baada y kingine ili ujue kipi hapendi sana au kinachomletea madhara ukichamganya sana hutoweza kujia kipi kimemdhuru kwa muda huo.

7.Usimlazimishe chakula mtoto mpe kidogo kidogo kwa mara nyingi akikataa kabisa badili aina ya chakula unachompa

8. Maji ni muhimu pia kwa mtoto kama ilivo kwa mtu mzima usisahau kumpa maji mwanao kila siku.

Maji ni uhai mpe uhai

9.Watu wengi wamekuwa wakisahau sana mboga za majani kwa watoto jitahidi kumpa mboga za majani mwanao.

10.Weka ratiba nzuri itakayowezesha mwanao kupata uwiano sahihi wa chakula chake mfano asubuhi anaweza kunywa uji baada ya saa mbili akanyonya baadae akalala akaamka akapewa chakula baada ya saa mbili ukampa juisi nk ipange upendavo la msingi ni kijitahidi ale kidogo lakini chenye faida.

Vyotew hivi vinapatikana katika maeneo yetu.


Report Page