Apple Yakubali, USB Type C Inakuja! #iPhone #iPad

Apple Yakubali, USB Type C Inakuja! #iPhone #iPad

https://teknolojia.co.tz/apple-yakubali-usb-type-c-inakuja-iphone-ipad/?utm_source=rss&utm_medium=rss&utm_campaign=apple-yakuba


Licha ya kuwa kwa sasa vifaa vingi sana vinatumia teknolojia ya kuchajia ya USB tena ile ya Type-C lakini bado si kwao Apple na hili wamelithibitisha wao kwamba linakwenda kubadilika.



Kwa taarifa iliyo rasmi kabisa Apple imekiri kuwa itaanza kutumia chaja zenye tundu hilo –jipya kwao – japokuwa timu nzima haina furaha kutokana na uamuzi huo.


Unaweza ukawa unajiuliza ni kwanini kampuni hii inalazimika kufanya maamuzi ambayo hata wao wenyewe hawayapendi (hawafurahishwi nayo) lakini utagundua ni kwamba kinachofanya hivyo ni sharia/maamuzi ambayo yamewekwa na nchi za ulaya.


Kwa nchi za ulaya imepitishwa kwamba wawe wanatumia USB Type-C katika simu zote, tabiti zote na kamera zote na hii ni mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2024.


SOMA PIA  Simu 20 Zilizouzika Zaidi Duniani Hadi Sasa-Namba 10 hadi 1
USB Type C, USB-C isolated on white background with clipping path

Na hili kuna hati hati kubwa likawezeshwa mpaka katika kompyuta mpakato (laptop) zote mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2026.


Kwa haraka haraka jambo hili linasaidia hata katika swala zima la kupunguza uchafu wa kielektroniki katika mazingira na vile vile inasaidia watu kuwa na machaguo ya muda mrefu.


Licha ya Apple kuwa mbishi kwa kipindi cha muda mrefu sana katika kuhakikisha kuwa anajitegemea kwa kila kitu safari hii hana ujanja tena, inabidi tuu aendane na hali halisi


SOMA PIA  Kampuni za simu Uchina zafanya vizuri kimauzo

Ningependa kusikia kutoka kwako, wewe unadhani ni sawa kwa kampuni ya Apple kuingia na kuanza kutumia chaja zile za USB Type-C?


Kumbuka Kutembelea Mtandao Wako Wa TeknoKona Kila Siku, Kwani Daima Tupo Nawe Katika Teknolojia!.


Nifuate Kwenye Mitandao Yangu Ya Kijamii


Instagram | Facebook | Twitter | LinkedIn


Hash



Report Page